Manchester United walishindwa 2-1 ugenini Sunderland Jumamosi na sasa wamo alama sita nyuma ya klabu nne zinazoongoza Ligi ya Premia.
Alipoulizwa baada ya mechi hiyo iwapo kuna matumaini kwa United kumaliza katika nafasi nne za kwanza, Van Gaal alisema: “Itakuwa vigumu sana.
Tangu msimu uliopita, washindi wa Europa League wamekuwa wakizawadiwa nafasi ya kucheza Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya wakiingia hatua ya kufuzu kabla ya hatua ya makundi au hatua ya makundi.
Van Gaal hata hivyo amesema hajapoteza matumaini ya kumaliza katika nne bora ligini.
United watacheza mechi ya mkumbo wa kwanza Europa League hatua ya 32 bora dhidi ya klabu ya Denmark FC Midtjylland Alhamisi.
No comments:
Post a Comment