Spurs wako Pointi 5 nyuma ya Leicester City huku Mechi zikiwa zimebaki 4 tu.
Chelsea ambao ndio walikuwa Mabingwa Watetezi wa BPL wataivaa Spurs Mei 2 Uwanjani Stamford Bridge na pia Leicester City hapo Mei 15 ambayo ndio Siku ya mwisho ya Msimu wa Ligi.
Aliongeza: "Tunaombea Leicester watwae kwa sababu wamestahili Msimu huu. Tuna Gemu nzuri Wiki ijayo dhidi ya Tottenham na kama tukiwafunga itakuwa vyema!”
Msimamo wa Hazard umeungwa mkono na Kiungo wa Chelsea Cesc Fabregas, ambae aliwahi kuwachezea Mahasimu wakubwa wa Tottenham wa London Kaskazini Arsenal kati ya 2003 na 2011, ambae pia anataka Leicester kutwaa Ubingwa kabla Chelsea hawajakutana na Tottenham.
Fabregas amesema: “Naamini Leicester watatwaa kabla ya hapo. Sitaki Spurs watwae Ubingwa lakini nadhani Leicester watautwaa na wanastahili!”
No comments:
Post a Comment