BAO 3 za Kipindi cha Pili ndani ya Dakika 6 zimeweka hai matumaini ya Tottenham ya kuwakamata Vinara wa BPL, Ligi Kuu England, Leicester City, walipoichapa Man United Bao 3-0 huko White Hart Lane Jijini London hii Leo.
Huu ni ushindi wa kwanza kwa Tottenham dhidi ya Man United tangu 2001 Uwanjani hapo na umewaweka wakiwa Nafasi ya Pili Pointi 7 nyuma ya Lecester.
Kipigo hiki kimewaacha Man United Nafasi ya 5 wakiwa Pointi 4 nyuma ya Timu ya 4 Man City na kuyafanya matumaini yao kucheza UEFA CHAMPIONS LIGI Msimu ujao kufifia na pia kulianzisha upya sakata la Mashabiki kumtaka Meneja Louis van Gaal ang’oke.
No comments:
Post a Comment