Katika Mechi hiyo Vardy alionyeshwa Kadi ya Njano ya pili na Refa Jon Moss kwa madai ya kujiangusha ndani ya Penati boksi na hivyo kutolewa nje kwa Kadi Nyekundu.
Vardy, mwenye Miaka 29 na ambae ameichezea England mara 6 chini ya Hodgson, amefungiwa Mechi 1 kwa Kadi hiyo.
Lakini huenda akafungiwa zaidi baada ya FA ya England kuamua kumfungulia Mashitaka ya Utovu wa Nidhamu kutokana na kumvaa Refa Moss kwa maneno makali mara baada ya kutolewa.
Hodgson ameeleza: "Nadhani Beki wa West Ham (Angelo Ogbonna) alimgusa kidogo na kutokana na spidi yake kali alikosa balansi!"
No comments:
Post a Comment