Toure aliumia Musuli za Mguuni Jumamosi kwenye Mechi ya Ligi Kuu England wakati Citu inaibonda Stoke City 4-0 na kukosekana kwake kumethibitishwa na Meneja wa City, Manuel Pellegrini.
Kukosekana kwa Toure kunatoa mwanya kwa Viungo Wawili wa Brazil Fernando na Fernandinho kuchezeshwa pamoja kama alivyodokeza Pellegrini.
Kutoka huko Madrid, Kocha wa Real, Zinedine Zidane, amebeba Kikosi chake chote kusafiri kwenda Jiji la Manchester akiwemo pia majeruhi Cristiano Ronaldo ambae Jumamosi hakucheza Mechi ya La Liga ambayo Real ilicheza Ugenini na Rayo Vallecano na kutoka nyuma 2-0 na kushinda 3-2.
No comments:
Post a Comment