
ROBO FAINALI
Marudiano Saa 3 Dakika 45 Usiku
Jumanne Aprili 12
Manchester City v Paris St-Germain [2-2]
Real Madrid v Wolfsburg [0-2]
Jumatano Aprili 13
Benfica v Bayern Munich [0-1]
Atletico Madrid v Barcelona [1-2]

Man City watatinga Uwanjani kwao Etihad, Jijini Manchester kuivaa Paris St-Germain huku Timu hizo zikiwa Sare ya 2-2 baada ya Mechi ya kwanza na Meneja wa City, Manuel Pellegrini, kudai Kepteni wake Kompany hayuko fiti kwa Asilimia 100 kucheza Mechi hii.
HUKO Santiago Bernabeu, ambako Real Madrid wako kwenye kauli mbiu ‘REMONTADA’ ikimaanisha kutoka nyuma na kupindua kipigo, wako kwenye kibarua kigumu cha kugeuza kichapo cha 2-0 toka VfL Wolfsburg walichopewa Wiki iliyopita lakini matumaini makubwa kwao ni kupona kwa Straika wao Karim Benzema.
Sasa Benzema yuko fiti kuungana na Safu ya Real ya mashambulizi wakiwamo Cristiano Ronaldo na Gareth Bale huku Kocha wao Mkuu, Lejendari Zinedine Zidane, akiishauri Timu yake kutumia akili zaidi, kujituma zaidi na kupigania kila Mpira ili wazoe ushindi.

No comments:
Post a Comment