
Jumamosi Liverpool watawakaribisha Mabingwa Watetezi wa England Leicester City kwenye Mechi ya EPL ambayo itatanguliwa na Ufunguzi rasmi wa Jukwaa Kuu jipya ambao Mmiliki Mkuu wa Klabu hiyo kutoka Kampuni ya Kimarekani Fenway Group, John W Henry, Mwenyekiti Tom Werner na Rais Mike Gordon watahudhuria.
-Kupanuliwa kwa Jukwaa Kuu la Anfield kutaiongezea Mapato Liverpool kwa Siku za Mechi kwa kiwango cha Pauni Milioni 20 hadi 30 kwa Msimu.
-Kabla, Liverpool walikuwa wakivuna Pauni Milioni 59 tu.
-Manchester United ndio wanaovuna kiwango cha juu kabisa cha zaidi ya Pauni Milioni 100.
Jukwaa Kuu la Anfield litaongeza Viti 8,500 na kuufanya Uwanja huo sasa upakie Watazamaji 54,000.
No comments:
Post a Comment