Mourinho ameeleza: "Sina la kusema kuhusu Wachezaji wangu lakini nawaonea ruhuma kwani hiyo ni kama tumefungwa wakati Arsenal wanaona wameshinda!"
Aliongeza: "Sare hizi na Burnley, Stoke na Arsenal ni kupoteza Pointi 9. Tungepata Pointi 6 tu tuko 4 Bora na karibu ya kileleni! Tunajua hivi sasa sie ndio Timu isiyo na bahati kwenye EPL!"
Man United wameshapambana na Manchester City, Liverpool, Chelsea na Arsenal bila ushindi wakitoka Sare 3 na kufungwa na Chelsea tu.
Hivi sasa wapo Nafasi ya 6 wakiwa Pointi 5 nyuma ya Arsenal ambao wako Nafasi ya 4 na ambao wapo Pointi 2 nyuma ya Vinara Liverpool.
No comments:
Post a Comment