

Newcastle, chini ya Meneja Rafael Benitez, wanaungana na Brighton kutinga moja kwa moja EPL na kubakiza Nafasi 1 itayogombewa na Timu zitakazomaliza Nafasi za 3, 4, 5 na 6.

Nafasi za 3 hadi za 6 zinashikwa na Reading, 79, Sheffield Wednesday, 78, Huddersfield, 78, na Fulham, 76.
Leeds United, ambao wako Nafasi ya 7 wakiwa na Pointi 73, wanaweza pia kuingia Kundi hilo la Mechi za Mchujo.
Kikosi cha Rafael Benitez kimekuwa kikisuasua katika Mechi zao za hivi karibuni kwa kambua Pointi 1 tu katika Mechi 3 zilizopita lakini ushindi wa Jana ulipokewa kwa furaha kubwa na Mashabiki 50,000 waliorundika Saint James Park.
No comments:
Post a Comment