BUKOBA SPORTS

Wednesday, April 26, 2017

SPURS KUWALINDA MASTAA WAKE


Tottenham itahakikisha Mastaa wao wote wanabakia Klabuni hapo na kuwauza tu wale ambao hawawahitaji kwa mujibu wa Meneja wao Mauricio Pochettino.
Spurs, ambao wako Nafasi ya Pili kwenye EPL, Ligi Kuu England, wanasakamwa na Klabu nyingine zinazowawinda Mastaa wao wakubwa wanaofanya vizuri Msimu huu.
Lakini Pochettino ambae amedai Mwenyekiti wa Klabu Daniel Levy wana uhusiano mzuri amesema Mkuu huyo amemhakikishia hawatauza Staa wao yeyote kwa sababu hawana shida na Fedha.
Pochettino amesisitiza: "Wachezaji tunaotaka wabaki watabaki!"
Miongoni mwa wanaosakwa na Klabu pinzani huko England ni Mabeki Kyle Walker na Danny Rose, Viungo Christian Eriksen na Dele Alli na Fowadi Harry Kane.
Wanyama

No comments:

Post a Comment