
Sanchez, Mchezaji wa Kimataifa kutoka Chile ambae Majuzi Jumapili aliifungia Arsenal Bao la ushindi walipowafunga Man City na kutinga Fainali ya FA CUP, amebakiza Mwaka mmoja tu kwenye Mkataba wake wa sasa huku akigomea kusaini Mkataba mpya.
Wenger ameeleza: "Sidhani kama unaweza kumuuza kwa Klabu nyingine ya Ligi Kuu England, huo ndio ukweli! Lakini kama nlivyosema nadhani atabaki na kusaini Mkataba!"
Ingawa yeye binafsi hajathibitisha kubaki Arsenal kwa Msimu ujao huku Mkataba wake ukiisha Juni, Wenger amesisitiza anashughulikia ununuaji Wachezaji wapya kwa ajili ya Msimu ujao.
No comments:
Post a Comment