BUKOBA SPORTS

Sunday, June 4, 2017

ARSENE WENGER ATAJA WAPYA ATAOSAINI, RIYAD MAHREZ NDANI YAKE!

Arsene Wenger ametoboa kuwa anapanga Kusaini Wachezaji wapya wasiozidi Watatu katika kipindi cha kuelekea Msimu Mpya wa 2017/18 utakaoanza Agosti 12.
Mapema Wiki hii, Wenger alisaini Mkataba Mpya wa kubakia Arsenal kama Meneja wa Miaka Miwili na hilo limechangia na kuhusishwa na kusaini Wachezaji Wapya

Mwenyewe Wenger amekiri kumtaka Winga wa Leicester City Riyad Mahrez.

Akihojiwa na TV ya beIN SPORT, Wenger amesema hatasaini zaidi ya Wachezaji Watatu.

Ameeleza: “Nasema Watatu hivi!”
Pia Wenger alifafanua kuwa Mastaa wake Mesut Ozil na Alexis Sanchez hataondoka Arsenal licha kuhusishwa na kuhama katika kipindi hiki.

Wawili hao wamebakisha Mwaka Mmoja katika Mikataba yao na wote wanasita kusaini Mikataba Mipya na hilo limechangia kuhusishwa kwao na kuondoka Arsenal.

Lakini Wenger amesisitiza kuwa Wachezaji hao watabaki Klabuni hapo na mazungumzo yataendelea kuhusu Mikataba yao Mipya.

No comments:

Post a Comment