
Katika mchezo huo wenyeji Chelsea walifunga goli la kwanza kupitia kwa Antonio Rudige kufuatia krosi ya Mbrazil Willian kisha baadaye Danny Drinkiwater akaongeza goli la pili kisha Pedro akafunga la tatu.
Willian aliongeza goli la nne kwa mkwaju wa penati baada ya kuchezewa rafu na Geoff Cameron na katika dakika ya 88 Zappacosta akakamilisha karamu ya magoli kwa kufunga goli lake la kwanza katika Ligi Kuu ya Uingereza.


Danny Drinkwater akifunga kwa shuti la kuubetua mpira kwenye kona ya goli.
No comments:
Post a Comment