
Crystal Palace licha ya kutoa sare tasa na vinara wa ligi Manchester City, pia ingeweza kuibuka na ushindi wa goli moja lakini kipa Enderson aliwanyima ushindi.
Palace walidhani kuwa wataibuka na ushindi baada ya kupata penati dakika za mwisho baada ya kuangushwa Wilfred Zaha lakini penati ya Luka Milivojevic ilipanguliwa.
Licha ya kutibuliwa rekodi ya ushindi mfululizo Manchester City pia imejikuta ikikumbwa na hofu ya majeruhi baada ya Kevin De Bruyne na Gabriel Jesus kuumia.


No comments:
Post a Comment