Thursday, January 25, 2018

CARABAO: ARSENAL 2 vs 1 CHELSEA, BLUES WATUPWA NJE! SASA FAINALI NI MAN CITY USO KWA USO NA ARSENAL


Kocha Arsene Wenger amesema kikosi chake kinacheza kwa ufasaha kufuatia kuondoka kwa Alexis Sanchez, baada ya Arsenal kutokea nyuma na kuifunga Chelsea magoli 2-1 katika kombe la Carabao, na kutinga fainali dhidi ya Manchester City.
Nacho Monreal, whose initial header sparked a double deflection off Marcos Alonso and Rudiger, wheels away to celebrateBaada ya timu hizo kutoka sare tasa katika mchezo wa kwanza Eden Hazard aliifanya Chelsea kuongoza kupata goli lakini goli la kujifunga la Antonio Rudiger likasawazisha na kisha Granit Xhaka akafunga goli la ushindi.

Ushindi huo umekuja ikiwa ni siku mbili tu kupita tangu mshambuliaji wake nyota Sanchez kuhamia Manchester United wakibadilishana na Henrikh Mkhitaryan ambaye Manchester United imemtoa ili kufanikisha dili.
Eden Hazard akiifungia Chelsea goli la kuongoza katika mchezo huo
Granit Xhaka akifunga goli la ushindi la Chelsea kwa mpira wa kuubetu.

No comments:

Post a Comment