BUKOBA SPORTS

Monday, January 29, 2018

LA LIGA: LIONEL MESSI AIPATIA USHINDI TIMU YA BARCELONA BAO 2-1 DAKIKA ZA LALA SALAMA.


Mchezo wa kwanza wa Philippe Coutinho katika La Liga akiwa na Barcelona umemalizika kwa ushindi wa magoli 2-1 baada ya Barcelona kutokea nyuma na kuifunga Alaves.
Mshambuliaji wa zamani wa Manchester City John Guidetti aliandika goli la kwanza kwa mpira uliomshinda kipa Marc-Andre ter Stegen na kuwafanya wageni Alaves waongoze.
Luis Suarez aliisawazishia Barcelona goli hilo na kisha baadaye Lionel Messi kuihakikishia ushindi kwa goli la mpira wa adhabu.


Mpira wa adhabu uliopigwa na Lionel Messi ukielekea kuwapita mabeki na kujaa wavuni.

No comments:

Post a Comment