BUKOBA SPORTS

Monday, January 29, 2018

MANCHESTER CITY NA CHELSEA ZASHINDA MECHI ZA KOMBE LA FA

Manchester City imetinga kilaini katika raundi ya tano ya Kombe la FA kwa kuibuka na ushindi wa magoli 2-0 dhidi ya timu ya Cardiff City.
Kevin de Bruyne aliipatia Manchester City goli la kwanza katika kipindi cha kwanza na Raheem Sterling akaongeza la pili kipindi cha pili.
Mpira uliopigwa na Kevin de Bryune ukitinga wavuni na kuandi goli la kwanza
Kocha Antonio Conte amemuelezea Michy Batshuayi kama mchezaji kijana mwenye fursa ya kung'ara baada ya kufunga magoli mawili, Chelsea ikishinda magoli 3-0 dhidi ya Newcastle.

Mshambuliaji huyo Mbelgiji amekuwa hapati nafasi katika kikosi cha Conte, ambaye alisema mchezaji huyo anaweza kuondoka kwa mkopo mwezi huu. Marcos Alonso alifunga la tatu.
Mchezaji kijana wa Chelsea Michy Batshuayi akifunga goli kwa kuupiga mpira kwa kuubetua

No comments:

Post a Comment