BUKOBA SPORTS

Saturday, February 3, 2018

FULL TIME: MANCHESTER UNITED 2 vs 0 HUDDERSFIELD, ALEXIS SANCHEZ AANZA KUFUNGA BAO OLD TRAFFORD.


Sanchez leo ameifungia bao kwa mkwaju wa penati Man United na kufanya mtanange kipindi cha pili kubadilisha matokeo na kuumaliza kwa bao  2-0 dhidi ya Timu ya iliyopanda Daraja msimu huu 2017/18 ya Huddersfield. Bao la kwanza lilifungwa na Lukaku dakika ya 55 na bao la pili akafunga Sanchez kwa mkwaju wa penati dakika ya 60. kwa matokeo hayo Man United wamebaki nafasi ya pili wakiwa na alama 56 huku kileleni akisimama Man City mwenye alama 69.


Sanchez akipongezwa na  Paul Pogba aliyeingia kipindi cha pili

Romelu Lukaku akitupia kambani dakika ya 55

Lukaku alipata pasi kutoka kwa Juan Mata na kufunga bao hilo kipindi cha pili

Lukaku akipongezwa na Jesse Lingard pamoja na Alexis Sanchez

No comments:

Post a Comment