BUKOBA SPORTS

Thursday, February 1, 2018

MAN UNITED NA CHELSEA ZACHEZEA VICHAPO ENGLAND EPL


Kocha Mauricio Pochettino ameipongeza Tottenham kwa kupambana kishujaa na kupata goli ndani ya sekunde 11 la Christian Eriksen lililosaidia ushindi wa magoli 2-0 dhidi ya Manchester United katika dimba la Wembley.
Baada ya goli hilo Manchester United walijaribu kutaka kusawazisha huku Jesse Lingard akikosa goli, lakini Phil Jones alizamisha jahazi baada ya kujifunga la pili akitumbukiza krosi ya
Kieran Trippier.

Christian Eriksen akifunga goli la kwanza ndani ya sekunde 11 tu ya mchezo
Kocha Eddie Howe amesema Bournemouth imepata ushindi bora kuwahi kuupata dhidi ya mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya Uingereza baada ya kuibuka na ushindi wa magoli 3-0 dhidi ya Chelsea.
Bournemouth ilipata magoli yake hayo katika kipindi cha pili kupitia kwa Callum Wilson, Junior Stanislas na Nathan Ake na kuipatia timu hiyo ushindi wake wa kwanza wa ugenini katika michezo saba.
Nathan Ake akifunga goli la tatu lililowamaliza kabisa Chelsea
 Romelu Lukaku kidogo afunge bao kipindi cha pili lakini alikuwa tayari kajenga kibanda!!

Alexis Sanchez akiteta jambo na Martial
Sanchez akiwekewa kigingi na mshambuliaji wa Spurs Harry Kane
Mourinho akiteta jambo na  Paul Pogba

No comments:

Post a Comment