Friday, May 18, 2018

TASWIRA MWANANA ZA BARABARA YA KARAGWE-KYAKA-MKOANI KAGERA


Muonekano wa eneo la Mlima Kishoju uliopo kwenye barabara Karagwe hadi Kyaka mkoani Kagera ambayo barabara hiyo ni sehemu ya barabara kuu ya Kyaka – Bugene – Kasulo yenye urefu wa kilometa 183.1 ambayo inaiunganisha Tanzania na nchi jirani za Rwanda na Burundi.
Picha Na-Faustine Ruta.




Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli aliifungua barabara hiyo ya Lami tarehe 07 Novemba, 2017 yenye urefu wa kilometa 59.1 iliyogharimu Shilingi Bilioni 81.597 fedha zote zikiwa zimetolewa na Serikali ya Tanzania na imejengwa na kampuni ya CHICO ya China.







No comments:

Post a Comment