“Kikosi changu kiko vizuri na kina uwezo wa kushinda mechi yoyote inayokuja mbele yake hata ya marudiano dhidi ya Al Ahly Shandy itakayofanyika Sudan,” alisema.
Simba inakabiliwa na mechi ya marudiano ya raundi ya tatu ya michuano ya Kombe la Shirikisho dhidi ya timu hiyo inayotarajiwa kufanyika Sudan katikati ya mwezi huu ambapo timu hiyo imejiweka kwenye mazingira mazuri ya kusonga mbele baada ya kushinda mabao 3-0 katika mechi iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
"Nina imani na kikosi changu kutokana na hali iliyokuwa nayo...nina uhakika kitafanya vizuri dhidi ya Yanga na hata katika mchezo ujao wa Kombe la Shirikisho," alisema Cirkovic.
No comments:
Post a Comment