BUKOBA SPORTS

Monday, June 11, 2012

EURO 2012: ITALI NA HISPANIA WAANZA MASHINDANO KWA SARE

Mabingwa wa Dunia Uhispania imeanza utetezi wa Kombe lao la ubingwa wa mashindano ya Ulaya kwa sare ya 1-1 dhidi ya Italia katika pambano la kundi C mjini Gdansk.
 
Italia ndiyo iliyotangulia baada ya kipindi cha kwanza kumalizika bila bao lolote kufungwa na alikua Antonio Di Natale aliyeingia badala ya Balloteli kufunga bao katika dakika ya 60.
 
Dakika nne baadaye Mabingwa wa Dunia na Ulaya walifumania lango la Italia na licha ya juhudi na umahiri wa Mabeki David Silva alimuona Cesc Fabregas na kumuwekea pasi maridhawa na bila kufanya makosa akaupenyeza mpira kumpita goli wa Italia Buffon.
Matokeo hayo yanaliweka kundi la C wazi ambapo Italia na Uhispania zinaondoka zote zikiwa na pointi moja.
Kabla ya mashindano haya wadadisi walionelea kama Uhispania itakabiliwa na kibarua kigumu kutetea taji lake kutokana na wachezaji wake wengi kuwa wachofu mno. Jumla ya wachezaji 23 wa timu hii ya Taifa wamecheza jumla ya dakika 89,884 katika msimu uliopita ikilinganishwa na wenzao walioshiriki kwa upungufu wa dakika 17,000.
Timu mbili zilizomo kwenye kundi la C Jamhuri ya Ireland na Croatia lazima zimeridhishwa na matokeo haya zikiona kua na fursa ya kufanya vyema na uwezekano mkubwa wa kufuzu kutoka michuano ya makundi.
Frustrated: Mario Balotelli missed a glorious opportunity by dilly-dallying with the ball
 Mario Balotelli naye alikosa bao muhimu sana
Mess: Fernando Torres made a hash of his chances
 Fernando Torres alikosakosa sana na alikuwa na nafasi nyingi za kufunga
Taking names: Georgio Chiellini is booked
 Georgio Chielliniakipewa kadi ya njano
Slick: Pirlo and Xavi Hernandez are two accomplished performers
 Pirlo na Xavi Hernandez wakichuana jana
Share: Eventually the spoils were split
Share: Eventually the spoils were split
Big saves: Iker Casillas made a couple of stunning stops
 VIKOSI
SPAIN: Casillas; Arbeloa, Ramos, Pique, Alba; Alonso, Busquets; Silva, Xavi, Iniesta; Fabregas
Akiba: Valdes, Albiol, Javi Martinez, Juanfran, Pedro, Torres, Negredo, Mata, Llorente, Santi Cazorla, Jesus Navas, Reina.
ITALY: Buffon; Bonucci, De Rossi, Chiellini; Maggio, Motta, Giaccherini, Pirlo, Marchisio; Cassano, Balotelli
Akiba: Sirigu, Ogbonna Obienza, Balzaretti, Abate, Di Natale, Barzagli, Borini, Montolivo, Giovinco, Diamanti, Nocerino, De Sanctis.
REFA: V Kassai (Hungary).

RATIBA MECHI ZINAZOFUATA:
Jumatatu, Juni 11
KUNDI D
Donetsk, Ukraine
[Saa 1 Usiku]
France v England
Kiev, Ukraine
Saa 3 Dak 45 Usiku
Ukraine v Sweden

No comments:

Post a Comment