Andy Murray, mchezaji bora zaidi wa kiume katika mchezo wa tennis nchini Uingereza, amefanikiwa kuingia robo fainali, baada ya kumshinda Richard Gasquet wa Ufaransa katika mashindano ya French Open, uwanja wa Roland Garros.
Hata hivyo aliweza kujikakamua na kupata ushindi katika seti ya pili, kabla ya kumuondoa Gasquet kwa 1-6 6-4 6-1 6-2.
Murray sasa Jumatano atapambana na David Ferrer wa Uhispania katika kujitahidi kuingia nusu fainali.
No comments:
Post a Comment