“Natamani sana kucheza. Kwa upande wangu msimu huu ni muhimu sana kwangu kudhihirisha ubora wangu kwa timu yangu na mashabiki wa klabu hii na kuisadia Manchester kuendelea kutwaa vikombe.” Anderson aliongea na tovuti ya manutd.com
PORTO KUMUUZA MOUTINHO KWA PAUNDI MILIONI 31.
KLABU ya Porto imethibitisha kuwa inaweza kumuuza mchezaji wake Joao Moutinho lakini wameionya klabu ya Tottenham Hotspurs ambayo inamuwinda mchezaji huyo kuwa watatakiwa kulipa kiasi cha paundi milioni 31.5 kama wanamuhitaji kiungo huyo. Moutinho amekuwa mchezji tegemeo kwa klabu na nchi yake ambapo meneja mpya wa Spurs Andres Villas-Boas ambaye ameshawahi kumfundisha kiungo huyo mwenye miaka 25 ni chaguo lake kubwa analohitaji. Kwasasa kocha huyo bado hajafanya mawasiliano na Porto kuhusiana na mchezaji huyo lakini wameonyesha nia ya kumhitaji mchezaji huyo na wako tayari kuanza mazunguzo kuhusu kiwango hicho cha fedha kilichowekwa na porto. Meneja wa Porto Votor Pereira amesema kuwa bado hajazungumza na Villas-Boas kuhusiana na suala hilo lakini anaonekana kumtaka mchezaji huyo na wao wanamhitaji lakini katika soka kama ikifikia wakati kama huu timu inakuwa haina jinsi bali kumuuza na kuiletea faida klabu. Spurs inamuhitaji Moutinho ili kuziba pengo la Luka Modric ambaye anaweza kuondoka msimu huu baada ya vilabu vya Real Madrid na Paris Saint Germain zikiitafuta saini yake kwa udi na uvumba.
KEWELL ATEULIWA KUWA MWANAMICHEZO BORA WA KIPINDI CHOTE NCHINI AUSTRALIA.

NYOTA wa zamani wa klabu ya Liverpool na Leeds United, Harry Kewell amepigiwa kura nchini kwao Australia kuwa mchezaji bora ambao hajapata kutokea kwa nchi hiyo. Kewell alitunukiwa tuzo hiyo ambayo iliamuliwa kwa kura za wananchi na maoni ya jopo la wataalamu katika sherehe zilizofanyika Alhamisi jijini Sydney. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 33 ambaye kwasasa amerejea Uingereza baada ya kucheza msimu mmoja katika klabu ya Melbourne inayoshiriki Ligi Kuu nchini humo maarufu A-League, hakuwepo kupokea tuzo hiyo. Kewell amesema kuwa kitendo cha kutajwa kama mmoja wachezaji bora kuwahi kutokea nchini humo ni kitu ambacho kamwe hawezi kukisahau katika maisha yake na aliwashukuru wote waliofanikisha shughuli hiyo pamoja na mashabiki waliompigia kura. Kura zaidi ya 15,000 zilihesabiwa katika uchaguzi huo wakati jopo la wachezaji wa sasa na wazamani, watendaji na wachambuzi mbalimbali pia walisaidia zoezi hilo la kumchagua mshindi.
No comments:
Post a Comment