BUKOBA SPORTS

Sunday, July 22, 2012

MANCHESTER UNITED WAENDELEA KUTESA NA KULA BATA AFRICA KUSINI


Anderson na Fluffy

wachezaji wa Manchester United’
Kusafiri kwa mechi za majaribio huwa ni kazi ngumu na kujituma kuna kuwa kwingi ila kwa wachezaji wa Man United ni kula bata tu kwenda mbele.

wachezaji wa Manchester United’

Rio Ferdinand
Man United wapo Afrika kusini kwa ajili ya mechi zao za majaribio lakini raha kidogo pia yafaa hapa na pale.

Anderson na Javier Hernandez

Antonio Valencia na Fluffy
Sir Alex yeye alijiachia katika viwanja vya Golf ambako alikuwa na Scholes na Carrick. Huku wachezaji wengine wajiachia na manyoka ambayo yanapatikana Afrika Kusini mjini Durban.
Wachezaji kama Rio Ferdinand, Antonio Valencia na Anderson walikuwa wakicheza na nyoka aitwaye Fluffy, mwanzo wote walikuwa waoga mwanzoni ila Kijana ROBBIE BRADY ndiye alianzisha njia kwa wenzake katika kumshika na kumchezeaji nyoka huyo.


safari mbugani
Matukio hayo yote yalifanyika katika mbuga za wanyama za Phezulu Safari Park huku wanyama kama Twiga,Pundamilia na Nyumbu wakiwa kiliwazo kwa wachezaji hao wa Man United ambao wanajiandaa na msimu mpya.

Paul Scholes na Michael Carrick katika golf

Sir Alex Ferguson akiwa katika golf

No comments:

Post a Comment