BUKOBA SPORTS

Monday, November 5, 2012

BARCLAYS PREMIER LEAGUE: LIVERPOOL 1 VS NEWCASTLE 1, QPR 1 VS READING 1, ZOTE ZABANANA NA KUTOA DROO!

Katika Mechi mbili za Ligi Kuu England zilizochezwa leo, Liverpool na Newcastle walitoka 1-1 na pia matokeo kuwa kama hayo kwa Mechi kati ya QPR na Reading.
Liverpool 1vs Newcastle 1Wakicheza kwao Uwanjani Anfield, Liverpool wamefanikiwa kutoka sare ya Bao 1-1 na Newcastle ambao walimaliza Mechi hii wakiwa Mtu 10 baada ya Sentahafu wao Fabricio Coloccini kutolewa nje kwa Kadi Nyekundu kwa rafu mbaya kwa Luis Suarez.
Newcastle ndio waliotangulia kupata bao safi la Yohan Cabaye katika Dakika ya 43 lakini nae Luis Suarez alisawazisha kwenye Dakika ya 67 pia kwa bao zuri.
Matokeo haya yamewaacha Newcastle wakamate nafasi ya 10 wakiwa na Pointi 14 kwa Mechi 10 na Liverpool wapo nafasi ya 12 wakiwa na Pointi 11 kwa Mechi 10.

Steven Gerrard receives an award from Gary McAllister to mark his 600th appearance Wet and wild: Liverpool fans are soaked by a rogue sprinkler at half time
Wadau na wapenzi wa Liverpool walipata janga la bomba la maji hapa na kutokea mzozo wa hapa na paleSealed with a kiss: Suarez celebrates scoring Liverpool's equaliser at Anfield
Suarez akishangilia huku akibusu mkono kama kawaida yake usiku huu baada ya kupata goli.
Get off: Coloccini is ordered from the field by referee Anthony Taylor
Nje, Coloccini is shown red card by ref Anthony Taylor
VIKOSI:
Liverpool: Jones, Wisdom, Skrtel, Agger, Jose Enrique, Gerrard, Allen, Sahin, Fernandez Saez, Suarez, Sterling
Akiba: Gulacsi, Assaidi, Henderson, Coates, Downing, Carragher, Shelvey.
Newcastle: Krul, Anita, Steven Taylor, Coloccini, Santon, Perch, Cabaye, Gutierrez, Ben Arfa, Cisse, Ba
Akiba: Harper, Simpson, Williamson, Shola Ameobi, Obertan, Sammy Ameobi, Ferguson.
Refa: Anthony Taylor

QPR 1 Reading 1 Dakika ya 66 Bao la Djibril Cisse likiwanyamazisha wapenzi wa soka na wadau wa Reading.
Sare hii haikuzisaidia Timu zote hizi mbili ambazo zipo mkiani na bado zinasaka ushindi wao wa kwanza kwenye Ligi Msimu huu.
Reading ndio walitangulia kupata Bao katika Dakika ya 16 alilofunga Kaspars Gorkss baada ya kona ya Nicky Shorey kuleta kizaazaa golini.
One up: Kaspars Gorkss (centre) wheels away after firing his side into the lead after 16 minutes
Kaspars Gorkss (katikati)baada ya dakika 16 wakishangilia na wenzake baada ya goli kupatikana
QPR walisawazisha katika Dakika ya 66 kwa Bao la Djibril Cisse.
Matokeo haya yanawaacha Reading wakamate nafasi ya 18 wakiwa na Pointi 5 kwa Mechi 9 wakifuatiwa na QPR wenye Pointi 4 kwa Mechi 10 na mkiani wapo Southampton wenye Pointi 4 kwa Mechi 9.
Julio Cesar  akifanya vitu hapa

Kiti cha Moto: Mkuu wa QPR  Tony Fernandes, Mark Hughes na inaonekana kuna kukimbia kiti hapa.
Cisse: upiti hapa ....

Jamie Mackie (kushoto) akichuana na Sean Morrison
Jason Roberts akichuana na Armand Traore
Cisse alionekana kuwa ni neema jana kuipatia QPR goli
Mark Hughes akiangalia kama atapata ushindi kupitia hapa kwa mara ya kwanza na QPR
VIKOSI:
QPR: Julio Cesar, Bosingwa, Ferdinand, Nelsen, Traore, Mackie, Granero, Diakite, Taarabt, Hoilett, Cisse
Akiba: Green, Derry, Hill, Wright-Phillips, Onuoha, Zamora, Faurlin.
Reading: McCarthy, Gunter, Morrison, Gorkss, Shorey, McCleary, Leigertwood, Tabb, McAnuff, Roberts, Hunt
Akiba: Federici, Pearce, Pogrebnyak, Le Fondre, Kebe, Robson-Kanu, Cummings.
Refa: Michael Oliver

RATIBA MECHI ZIJAZO
Jumatatu, Novemba 5
[SAA 5 Usiku]
West Bromwich Albion v Southampton
Jumamosi, Novemba 10
[SAA 12 Jioni]
Arsenal v Fulham
Everton v Sunderland
Reading v Norwich City
Southampton v Swansea City
Stoke City v Queens Park Rangers
Wigan Athletic v West Bromwich Albion
[SAA 2 na Nusu Usiku]
Aston Villa v Manchester United
Jumapili, Novemba 11
[SAA 10 na Nusu Jioni]
Manchester City v Tottenham Hotspur
[SAA 12 Jioni]
Newcastle United v West Ham United
[SAA 1 Usiku]
Chelsea v Liverpool

No comments:

Post a Comment