MATOKEO:
Jumatano Novemba 7
Azam 1 JKT Oljoro 0
Coastal Union 1 Polisi Moro 0
Mtibwa Sugar 1 JKT Ruvu 0
Wakiwa kwao Uwanja wa Azam Complex
uliopo Chamazi kwenye Viunga vya Jiji la Dar es Salaam, leo Azam FC
wamefuta machungu ya kulambishwa Bao 2-0 na Yanga kwa kuwafunga JKT
Oljoro Bao 1-0 katika Mechi ya Ligi Kuu Vodacom, VPL, kwa Bao la
Mchezaji wao kutoka Ivory Coast, Kipre Tchetche.
MSIMAMO TIMU ZA JUU
1 Yanga Mechi 12 Pointi 26
2 Azam FC Mechi 12 Pointi 24
3 Simba Mechi 12 Pointi 23
4 Coastal Mechi 12 Pointi 22
Bao
hilo la Tchetche, aliefunga kwa Penati, limewafanya Azam wakamate
nafasi ya pili na kuwashusha Mabingwa watetezi Simba hadi nafasi ya 3.
Yanga bado wako kileleni wakiwa na Pointi 26.
Kwenye Mechi nyingine za Ligi
zilizochezwa leo, huko Mkwakwani, Tanga, Coastal Union wameifunga Polisi
Morogoro Bao 1-0 kwa bao la Daniel Lyanga na huko Manungu, Morogoro,
Mtibwa Sugar nao pia wameishinda JKT Ruvu kwa Bao 1-0 kwa bao la Issa
Rashid.
RATIBA MECHI ZIJAZO:
Jumamosi Novemba 10
Mgambo JKT v Azam (Mkwakwani, Tanga)
African Lyon v Mtibwa Sugar (Azam Complex, Dar es Salaam)
Jumapili Novemba 11
Simba v Toto Africans (Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam)
Coastal Union v Yanga (Mkwakwani, Tanga)
Tanzania Prisons v JKT Ruvu (Sokoine, Mbeya)
Kagera Sugar v Polisi Morogoro (Kaitaba, Kagera)
JKT Oljoro v Ruvu Shootings (Sheikh Amri Abeid, Arusha)
MECHI ZA VIPORO VYA PRISONS:
Jumatano Novemba 14
Mgambo JKT v Tanzania Prisons [Mkwakwani, Tanga]
Jumapili Novemba 18
Ruvu Shooting v Tanzania Prison [Mabatini, Pwani]
No comments:
Post a Comment