BUKOBA SPORTS

Monday, January 21, 2013

LA LIGA: VALENCIA 0 vs REAL MADRID 5, CRISTIANO RONALDO NA Di MARIA WATUPIA MBILI MBILI HUKU HIGUAIN AKIWAFUNGULIA NJIA!!

JANA, wakicheza ugenini na Levante, Real Madrid walishinda Bao 5-0 katika Mechi ya Ligi ya Spain, La Liga huku Nyota wao Cristiano Ronaldo na Angel Di Maria, wakipiga Bao 2 kila mmoja.
Ushindi huo wa Real umewafanya wafikishe Pointi 40 wakiwa Pointi 7 nyuma ya Timu ya Pili Atletico Madrid ambao jana waliifunga Levante Bao 2-0 kwa Bao za Adrian Lopez Alvarez, Dakika ya 32 na Koke, Dakika ya 60.
Atletico Madrid wako Pointi 8 nyuma ya Vinara Barcelona ambao juzi walipoteza Mechi yao ya kwanza ya La Liga Msimu huu baada ya kuchapwa 3-2 na Real Sociedad.

Cristiano Ronaldo akishangilia baada ya kufunga goli 36

 Angel Di Maria (kushoto) na Ronaldo wakishangilia baada ya kufunga magoli

Golikipa wa Valencia Diego Alves na difenda Adil Rami wakijaribu kuokoa mpira uliopigwa na Sami Khedira

 Michael Essien akichuana na mchezaji wa Valencia jana usiku

Victor Ruiz (kushoto), akijaribu kuukinga mpira usichukuliwe na mpizani wake.
VIKOSI:
Valencia: Diego Alves; Ricardo Costa, Rami, Victor Ruiz, Guardado; Gago (Barragan 45), Tino, Jonas, Banega, Piatti (Bernat 72); Soldado (Valdez 65)
Real Madrid: Casillas; Arbeloa, Varane, Albiol, Centrao; Khedira (Callejon 75), Alonso (Essien 58), Di Maria, Ozil (Modric 67), Cristiano Ronaldo; Higuain

MAGOLI:
Valencia 0 vs Real Madrid 5
-Gonzalo Higuain Dakika ya 9
-Angel Di Maria 34 & 45
-Cristiano Ronaldo 36 & 41


MATOKEO:
Jumapili Januari 20
Malaga 1 Celta Vigo 1
Osasuna 2 Deportivo La Coruna 1
Real Valladolid 2 Real Zaragoza 0
Atletico Madrid 2 Levante 0
Valencia 0 Real Madrid 5

No comments:

Post a Comment