BUKOBA SPORTS

Saturday, May 18, 2013

REAL MADRID YACHINJWA NA ATHLETICO MADRID KWA BAO 2-1 KWENYE FAINALI YA COPA DEL REY JANA USIKU, HUKU KOCHA MOURINHO NA RONALDO WAKIAMBULIA KADI NYEKUNDU!


Kazi kwisha, kocha mwenye ngebe nyingi na maneno mengi zaidi duniani, Mreno Mario Jose Dos Santos Ferlix Mourinho hatimaye amemaliza msimu wa 2012/2013 bila kikombe chochote baada ya usiku huu kupoteza mchezo wa fainali ya Copa Del Rey kwa kufungwa mabao 2-1 na wapinzani wake wakubwa katika mji wa Madrid, klabu ya Atletico Madrid.
Bao la dakika za majeruhi lililotiwa kambani na mchezaji wa Atletico Joao Miranda limeipa ushindi wa 2-1 na kuacha machungu makubwa kwa benchi la ufundi, wachezaji na mashabiki wa Real De Madrid ambao wamemaliza msimu bila taji lolote huku wapinzani wao wakubwa FC Barcelona wakiwa wameshatwaa ubingwa wa La Liga.
Katika mchezo huo, dunia imeshangazwa na kitendo cha Kocha Mourinho kupewa kadi nyekundu na mwamuzi Clos Gomez kufuatia kutoelewana lugha , huku baadaye nyota wa klabu hiyo Cristiano Dos Santos Aveiro Ronaldo naye akioneshwa kadi nyekundu baada ya kumfanyia madhambi mchezaji Gab.
Msumari wa Ushindi: Joao Miranda akitia kambani bao la pili na la ushindi kwa Atletico Madrid watoto wa mjini wanasema amepiga ndosi ya maana kuzamisha gozi kambani, si mchezo hiyo ndio kazi
Duuh! haamini kabisa: Haya ni kadi nyekundu kwa Cristiano Ronaldo, baada ya kumfanyia madhambi Gabi
Haya sasa!, ze spesho one: Mwamuzi Clos Gomez anamuonesha kadi nyekundu kocha wa Real Madrid Jose Mourinho

Ronaldo alikuwa wa kwanza kufunga bao la kuongeza katika dakika ya 55 na baadaye Diego Costa aliisawazishia Atletico Madrid akimalizia kazi nzuri iliyofanywa na nyota anayewindwa na Mmiliki wa Chelsea ,Roman Abramovich ili amsajili msimu ujao, Radamel Garsia Zarate Falcao.
Kipindi cha pili mchezo ulianza kwa Real Madrid kutafuta bao la pili, lakini bunduki zao ziligonga mtambaa panya mara tatu na kuoshwa kwa umakini mkubwa na walinzi wa Atletico.
Bao la ushindi la Miranda limewapa ushindi wa kwanza wa nyumbani Atletico Madrid tangu mwaka 1996.
Bonge la msumari: Diego Costa akiisawazishia timu yake huku kipa Diego Lopez akiambulia manyoya tu!
Basi la Real Madridi liliingia uwanjani kwa ngebe nyingi huko wakilakiwa na mashabiki wao

Si mchezo!: Kocha wa Atletico Diego Simeone akishangila bao la timu yake
Mwari huyooooooooo!! wa The Copa Del Rey, Real Madrid wameishia kunawa, hakuna kumgusa jamani!
Jose Mourinho akiwa jukwaani akihesabu siku za kuwa kocha wa Real Madrid
Sasa itakuwa njia nyeupe kwa Mourinho kuondoka Hispania na kurejea England huku ikisemekana atakapotua Chelsea anataka kumchukua Ronaldo ili kuimarisha kikosi chake, wakati huo Manchester United nao wanataka kumrejesha nyota wao huyo wa zamani.
Ronaldo chini ya ulinzi mkali, hapiti mtu, bora mpira upiteLuka Modric na Kokewakipandishiana jana usiku.
VIKOSI:

No comments:

Post a Comment