Kazi kwisha, kocha mwenye ngebe nyingi na maneno mengi zaidi duniani, Mreno Mario Jose Dos Santos Ferlix Mourinho hatimaye amemaliza msimu wa 2012/2013 bila kikombe chochote baada ya usiku huu kupoteza mchezo wa fainali ya Copa Del Rey kwa kufungwa mabao 2-1 na wapinzani wake wakubwa katika mji wa Madrid, klabu ya Atletico Madrid.
Bao la dakika za majeruhi lililotiwa kambani na mchezaji wa Atletico Joao Miranda limeipa ushindi wa 2-1 na kuacha machungu makubwa kwa benchi la ufundi, wachezaji na mashabiki wa Real De Madrid ambao wamemaliza msimu bila taji lolote huku wapinzani wao wakubwa FC Barcelona wakiwa wameshatwaa ubingwa wa La Liga.
Ronaldo alikuwa wa kwanza kufunga bao la kuongeza katika dakika ya 55 na baadaye Diego Costa aliisawazishia Atletico Madrid akimalizia kazi nzuri iliyofanywa na nyota anayewindwa na Mmiliki wa Chelsea ,Roman Abramovich ili amsajili msimu ujao, Radamel Garsia Zarate Falcao.
Kipindi cha pili mchezo ulianza kwa Real Madrid kutafuta bao la pili, lakini bunduki zao ziligonga mtambaa panya mara tatu na kuoshwa kwa umakini mkubwa na walinzi wa Atletico.
Bao la ushindi la Miranda limewapa ushindi wa kwanza wa nyumbani Atletico Madrid tangu mwaka 1996.
Si mchezo!: Kocha wa Atletico Diego Simeone akishangila bao la timu yake
Sasa itakuwa njia nyeupe kwa Mourinho kuondoka Hispania na kurejea England huku ikisemekana atakapotua Chelsea anataka kumchukua Ronaldo ili kuimarisha kikosi chake, wakati huo Manchester United nao wanataka kumrejesha nyota wao huyo wa zamani.
No comments:
Post a Comment