Usain Bolt, ambae ni Shabiki mkubwa wa Man United, Siku zote amekuwa akitaka kuichezea Klabu hiyo na mara nyingi alikuwa akimuomba Rafiki yake, Sir Alex Ferguson, Meneja aliestaafu wa Man United, ampe nafasi ya kuvaa Jezi ya Mabingwa hao
Wakati akimuomba Sir Alex Ferguson ili achezee Man United, Usain Bolt, alisema: “Najua nitaleta tofauti kwenye Timu. Nitakuwa Mtu mwenye kasi kupita wote Uwanjani lakini pia naweza kucheza!”
Mwezi uliopita, Ferguson alishamkubalia Bolt kuchezea Kikosi cha Malejendari wa Man United walipocheza na Real Madrid lakini mipango hiyo ilikufa baada ya Ferguson kustaafu.
Inaaminika Bolt atapata nafasi hii kucheza na Sevilla, baada ya Rio Ferdinand kumkingia kifua na Meneja David Moyes kulikubali ombi hilo.
Hivi Juzi, Bolt aliivunja Rekodi ya Michael Johnson ya Sekunde 20.01 kwenye Mbio za Mita 200 iliyodumu Miaka 23 baada ya yeye kutumia Sekunde 19.73 kwenye Mashindano ya Diamond League huko Jijini Paris.
No comments:
Post a Comment