BUKOBA SPORTS

Saturday, July 6, 2013

SVIONA NYAMEYO ATWAA TAJI LA REDD'S MISS TEMEKE 2013


Mshindi wa Redd's Miss Temeke 2013, Sviona Nyameyo (katikati), ambaye ni mwanafunzi wa mwaka wa kwanza wa Sheria Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), akiwa na mshindi wa pili, Narietha Boniface, mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Sayansi ya Tiba Muhimbili (MUHAS), na mshindi wa tatu, Latifa Mohamed ambaye ni muhitimu wa kidato cha sita baada ya kutangazwa washindi katika shindano hilo lililofanyika TCC Club Chang'ombe, Dar es Salaam

Bendi ya Twanga Pepeta ikitumbuiza katika mashindano hayo

Walimb wende wakionesha umahiri wa kucheza muziki

Majaji wa mashindano hayo, Albert Makoye, Dk. Lamesh Shah (katikati) na Lucas Lutha (kulia), wakifuatilia kwa makini.

Mgeni rasmi ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Temeke, Abbas Mtemvu akizungumza na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Jambo Concept Tanzania Limited, Juma Pinto.

Warembo wakiwa wamejipanga tayari kwa mashindano hayo

Redds miss Temeke waliofanikiwa kuingia tano bora

Mwandaaji wa shindano hilo, Benny Kisaka akitangaza washindi na zawadi watakazozawadiwa

Mshindi wa Pili

Mbunge wa Temeke, Abbas Mtemvu ambaye alikuwa mgeni rasmi akimkabidhi mshindi wa kwanza wa shindano hilo, Sviona Nyameyo zawadi ya sh.milioni 1.
Mkurugenzi wa Rio Gym $ Spa, Said Othman (kulia), akimkabidhi kadi itakayo muwezesha Mkurugenzi wa BMP Promotion, Beny Kisaka ambaye ni muandaaji wa mashindano ya Redd's Miss Temeke kuingia katika Gym hiyo kufanya mazoezi kwa kipindi cha mwaka mmoja baada ya kuwa muandaaji bora wa mashindano hayo kwa zaidi ya miaka 15. Gym hiyo ipo kwenye Jengo la Quality Centre Barabara ya Nyerere. Kadi hiyo imelipiwa sh. milioni 1.4.

Mkurugenzi Mtendaji wa Kiwanda cha Konyagi cha Tanzania Distilleries Limited< David Mgwassa (wa pili kulia) akijadiliana jambo na Mkurugenzi wa Masoko wa kiwanda hicho, Joseph Chibehe. Kiwanda hicho kimedhamini shindano hilo

No comments:

Post a Comment