BUKOBA SPORTS

Thursday, March 27, 2014

BANGO LA "THE CHOSEN ONE" UWANJANI OLD TRAFFORD LALETA KIZAAZAA UWANJANI!!! MASHABIKI WA UNITED WAMJIA JUU KOCHA DAVID MOYES! WAMPANGIA STAILI MPYA YA KUMUONDOSHA.

Kundi la mashabiki Manchester United linajiandaa kuchangisha fedha za kutosha kwa ajili ya kukodi ndege ambayo itapita juu ya paa la uwanja wa Old Trafford katika mchezo wa jumamosi ijayo dhidi ya Aston Villa – ikiwa na ujumbe wa kumsema kocha wao David Moyes.
Mashabiki hao ambao juzi kwenye mechi dhidi ya Manchester City walikuwa wakimtukana Moyes pamoja na kocha wa zamani wa klabu hiyo Sir Alex Ferguson na hata kufikia hatua ya kutaka kulishusha bango la kumsifu Moyes liliopo kwenye jukwaa la Stretford End – wanasema wanataka kuonyesha namna walivyochoshwa na kocha huyo.
Discontent: One supporter looks angry as he passes Moyes and his staffShabiki mmoja juzi wakati wa mtanange wao na City alimkalia vibaya Kocha David Moyes!!! Alikuwa akimtumia mabango ya hatari..akimtaka aondoke wamechoka mashabiki!! Akiwatuhumu na safu yake ya viongozi wake alionao!
Moyes kwa machungu ilibidi ajiinamie maana alikuwa hana la kufanya, Hakina inatakiwa mabadiliko pale Old Trafford.3-0 kutoka kwa Man City kwenye Uwanja wa Old Trafford kikiwa ni kipigo cha 6 Nyumbani.

Bango hilo la 'The Chosen One' limewekwa na Kundi maarufu la Washabiki wa Man United wanaokaa Jukwaa la Stretford End na wenyewe hujiita, Stretford End Flags, likiwa kama utambuzi wa chaguo la Meneja Mstaafu Sir Alex Ferguson kumteua David Moyes kumrithi. 
Mara baada ya Mechi na City kumalizika, Walinzi wa Uwanja wa Old Trafford ilibidi wakae kulinda Bango hilo lising’olewe.
WAKATI HUO HUO, Kundi rasmi la Washabiki wa Man United, Manchester United Supporters Trust (MUST), limeanika rasmi mawazo yao kuhusu hali ya sasa ya Washabiki na pia kuhusu David Moyes na Timu.

MUST, kupitia Msemaji wao Sean Bones, wamesema: “Ikiwa akili yako kwa Miaka 20 mfululizo imezoea ushindi tu na ghafla hupati tena, ni lazima utaathirika kiakili!”
Hata hivyo, MUST inaamini matatizo yote si kwa sababu ya Meneja pekee. 

MUST inaamini kutowekeza kwa Wamiliki wa Klabu, Familia ya Glazer, tangu wainunue Man United Mwaka 2005, ndio kitu kikubwa kimesababisha kwa Man United kushindwa vibaya Msimu huu. 
MUST wanaamini kugoma kwa Familia ya Glazer kushindana na Timu kama Man City katika Soko la Uhamisho kumewaacha dhaifu katika kugombea Ubingwa. 
Pia, MUST wamelalamika kuwa kwa kumruhusu Mkurugenzi Mtendaji, David Gill, kuondoka wakati mmoja na Sir Alex Ferguson lilikuwa ni kosa kubwa.


No comments:

Post a Comment