Ushindi huo wa Man City ni wa tatu mfululizo Uwanjani Old Trafford na jinsi walivyoshinda kulionyesha wazi jinsi gani Man United, chini ya Meneja David Moyes, ilivyoporomoka kwa kipindi kifupi.
Baadhi ya Wachambuzi wanadai kuwa Moyes amerithi Kikosi ambacho uchezaji wao umeshuka lakini wengi wanadai Meneja huyo hajui kupanga Timu na hilo limemfanya abadili Kikosi katika kila Mechi anayocheza kitu ambacho hakisaidii kabisa Uchezaji Kitimu kwani kila Siku una Timu mpya.
Wengine wanadai Moyes hana uzuri wa kuiongoza Man United lakini, Paul Scholes, Mchezaji wa zamani wa Man United, ametaka Meneja huyo apewe muda zaidi na pia asaidiwe mwishoni mwa Msimu kununua Wachezaji wapya.
No comments:
Post a Comment