Siku ya leo Dunia inasherekea siku ya wanawake ambayo huadhimishwa kila mwaka ifikapo tarehe 8 ya mwezi wa tatu kila mwaka na kauli mbiu ya mwaka huu ni Msukumo wa mabadiliko.
Sherehe hizi huadhimishwa na mataifa mbalimbali duniani kwa lengo la kuhakikisha dunia inafahamu wajibu na mchango wa mwanamke alionao kwenye jamii ya sasa.
Mataifa mengi ya Afrika zikiwemo nchi za ukanda wa Afrika mashariki zimekuwa zkiripoti unyanyasaji wa wanawake ambapo baadhi ya makabila yameendelea na mila za kukeketa wanawake jambo ambalo linapigwa vita na wanaharakati wa wanawake na Umoja wa Mataifa.
No comments:
Post a Comment