Castle Lager kupitia ushirikiano wake na FC Barcelona leo imezindua shindano la kitaifa la mpira wa miguu litakalohusisha wachezaji sita kila upande. Shindano hilo litakalojulikana kama “Castle Lager Perfect 6” litamalizika kwa kupata washindi ambao watatembelea uwanja wa Camp Nou na kujionea FC Barcelona ikicheza katika ziara ambayo itagharamiwa kila kitu na Castle Lager.
Castle Lager ikishirikiana na Chama cha Waandishi wa Habari wa Michezo (TASWA) wameandaa tamasha la Perfect Six Media Bonanza ikiwa ni sehemu ya uzinduzi wa shindano hili la kusisimua. Hii ni njia ya kuwaleta pamoja waandishi wa habari na kuwapa uelewa juu ya ushirikiano huu na pia ni fursa kwao wenyewe kushiriki na kujionea namna tukio hili ambalo litahusisha mamia ya Watanzania kwa muda wa miezi mitano mwaka huu linavyofanyika.
Akiongea kwenye uzinduzi jijini Dar es salaam leo, Meneja Masoko wa Kampuni ya Bia Tanzania, Fimbo Buttallah amesema shinano la Perfect Six limelenga kuzungumza na wanywaji wa Castle Lager ambao wana shauku ya kucheza mpira wa miguu, kuleta pamoja wanywaji wa Castle Lager kutoka baa mbalimbali ili wafurahie pamoja, kuongeza mauzo ya Castle Lager na kuwapa zawadi wateja wa bia hiyo. Katika kutambua mchango mkubwa wa vyombo vya habari, tumeamua kuzindua shindano hili na bonanza la waandishi wa habari.
“Hii itafatiwa na shindano litakalofanyika nchi nzima ambapo timu mbalimbali katika Kanda saba zitasajiliwa na kucheza katika hatua za mtoano kwenye maeneo mbalimbali ambayo yatachaguliwa na kutangazwa mapema. Kila kanda itatoa timu moja na kufanya jumla ya timu saba ambazo zitawakilisha Kanda hizo huku timu ya nane ikitoka kwenye vyombo vya habari. Timu hizo zitachuana kwa mtoano kwenye robo fainali, nusu fainali, na hatimaye fainali.
“Timu itakayoshinda itapata nafasi ya kipekee kwenda Hispania kutembelea uwanja wa Camp Nou na kujionea timu ya FC Barcelona ikicheza,” Buttallah aliongeza.
Tunachukua nafasi hii kuwahamasisha wanywaji wa Castle Lager kwamba Perfect Six itawafikia popote walipo kupitia bar mbalimbali hivyo waanze kuandaa timu zao. Vilevile tunaikaribisha timu ya waandishi wa habari itakayoshiriki ikiiwakilisha TASWA na ni matumaini yetu kwamba shindano hili litaleta msisimko mkubwa,” alisema Buttallah.
No comments:
Post a Comment