BUKOBA SPORTS

Wednesday, April 30, 2014

KATIBU MKUU FIFA JEROME VALCKE KUTUA DAR LEO HII MEI 1! KUFUNGUA SEMINA YA CECAFA, KUONGEA NA WANAHABARI!

Katibu Mkuu wa Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA), Jerome Valcke anawasili nchini LEO (Mei 1 mwaka huu) ambapo atafungua semina ya mawasiliano kwa nchi wanachama wa Baraza la Vyama vya Mpira wa Miguu Afrika Mashariki na Kati (CECAFA).
Valcke ambaye atafuatana na maofisa wengine saba wa FIFA baadaye leo hii (Mei 1 mwaka huu) atakuwa na mkutano na waandishi wa habari. Mkutano huo utafanyika saa 4 kamili asubuhi kwenye hoteli ya Double Tree by Hilton iliyopo Oysterbay, Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment