BUKOBA SPORTS

Saturday, April 12, 2014

FULL TIME - EPL, SUNDERLAND 0 v EVERTON 1, BAO LA USHINDI LA WES BROWN LAWAWEKA EVERTON NAFASI YA KUCHEZA UEFA!

Bao la Dakika ya 75 la kujifunga mwenyewe Wes Brown limewapa Everton ushindi wa Bao 1-0 walipocheza Ugenini huko Stadium of Light na kuwafanya waipiku Arsenal kwenye Nafasi ya 4 na kuiacha Sunderland ikiwa mkiani.

Bao hilo la kujifunga limetosha dakika 90 za mtanange na kutoka 1-0, Everton wakitoka wababe katika mchezo huo na Ushindi huu ukiwapandisha Everton nafasi ya nne wakiwatoa katika nafasi hiyo Arsenal. Wao Sunderland kipigo hicho kinawakandamizia zaidi mkiani.

No comments:

Post a Comment