Giggs aliteuliwa Siku ya Jumanne mara baada ya David Moyes kufukuzwa na Mkutano huo wa Leo utafanyika Saa 6 Mchana, Saa za Bongo, huko Aon Training Complex, Jijini Manchester ambako ndio Kituo cha Mazoezi cha Man United.
Pia, kama alivyokuwa Sir Alex Ferguson,
Giggs ameurudisha Mkutano huo wa kila Wiki wa Waandishi wa Habari,
unaofanyika kila Ijumaa, kufanyika Asubuhi kabla ya kuanza Mazoezi
wakati Moyes alikuwa akiufanya baada ya Mazoezi.
Mechi ya Kwanza ambayo Giggs atasimamia
kama Meneja, akisaidiwa na Nicky Butt, Paul Scholes na Phil Neville, ni
Jumamosi Uwanja wa Old Trafford dhidi ya Norwich City kwenye Ligi Kuu
England.
Tayari Giggs ameshawataka Wachezaji wake kurudia kucheza kama Manchester United kwa kuzishambulia na kuzibana Timu kama walivyokuwa wanafanya chini ya Sir Alex Ferguson.Giggs ataisimamia Man United kwa Mechi zao 4 za Ligi zilizobaki Msimu huu.
No comments:
Post a Comment