Habari za ndani ya Old Trafford zinasema kuwa mara baada ya Ryan Giggs kuteuliwa Meneja, aliwaambia Wachezaji wakati umefika wa kurudi kucheza kama Manchester United, kushambulia bila kuogopa Timu na kuzibana Timu bila kujali wao ni nani.
Nae Nicky Butt, ambae ndie alikuwa Kocha wa Timu ya Rizevu ya Man United, ameiambia MUTV, Kituo cha TV cha Man United, kuhusu Mechi yao na Norwich City kwamba: “Hii ni Gemu kubwa kwetu na fahari kubwa kwetu. Kuwa pamoja ni kitu kisichoaminika. Tuliingia hapa pamoja tukiwa na Miaka 12 na kwa sisi kuwa pamoja sasa ni fahari kubwa mno!”
Butt alisisitiza kuwa Man United inao Wachezaji wazuri mno ambao wanaijali Timu yao na wanaitakia mema Klabu yao.
No comments:
Post a Comment