
Kipa Schwarzer akipasha hapa tayari kwa mchezo wa kesho jumatano na Atletico Madrid

John Terry

Kocha Jose Mourinho akiangalia vijana wake

Kipa Petr Cech ndani na kapona...

Kazi ipo kesho kwenye marudiano

Katika Mashindano ya UEFA, Chelsea wamefungwa mara 2 tu kati ya 7 ambazo walitoka Sare Ugenini. Wakitoka Sare 0-0 Ugenini, Chelsea wameshinda mara 1 tu na kufungwa mara 2 na hivi karibuni ni pale walipotolewa na Barcelona kwenye Nusu Fainali ya 2008/09 walipotoka 0-0 huko Nou Camp na kufungana 1-1 Stamford Bridge.
Chelsea wameshinda mara 1 tu kati ya 4 walizokutana Nusu Fainali na Klabu toka Spain na hiyo moja ilikuwa dhidi ya Barcelona Msimu wa 2011/12. Mwaka 2009 walitolewa na Barcelona, 1998/99 walitolewa na RCD Mallorca kwenye Kombe la Washindi la UEFA na 1994/95, walibwagwa na Real Zaragoza.
Atletico, ambao wamefuzu mara zote mbili baada kutoka Sare 0-0 Nyumbani, wameshinda mara 1 tu Ugenini dhidi ya Klabu za England kati ya Mechi 9. Mara hiyo 1 ni pale walipoifunga Leicester City FC Msimu wa 1997/98 kwenye Raundi ya Kwanza ya UEFA Cup.

John Terry kwenye mazoezi na Cesar Azpilicueta, Gary Cahill, Frank Lampard pamoja na Tomas Kalas
No comments:
Post a Comment