BUKOBA SPORTS

Monday, May 12, 2014

BALAA!! CHANGAMKIENI FURSA HII!! ASTON VILLA IPO SOKONI!!

WAKATI MMILIKI wa Aston Villa akitoboa kuwa anaiuza Klabu hiyo na Mwenyekiti wa Southampton akikubali Chipukizi wake wanaocheza England wanasakwa na Klabu kubwa, Mabingwa wa zamani wa England, Manchester United, wameanza kutafakari athari za kukosa kucheza Mechi za Klabu Barani Ulaya Msimu ujao.
MMILIKI wa Aston Villa, Randy Lerner, amesema umefika wakati muafaka kwa Klabu hiyo kutafuta njia mbadala baada ya kuiweka Sokoni kuiuza Klabu hiyo.
Aston Villa fans
Lerner, ambae ni Mfanyabiashara wa Kimarekani alieinunua Villa Mwaka 2006 kutoka kwa Doug Ellis ambae aliimiliki Villa kwa muda mrefu, ameamua kuiuza Klabu hiyo baada Msimu huu kumaliza ikiwa Nafasi ya 15 kwenye Ligi Kuu England.

No comments:

Post a Comment