BUKOBA SPORTS

Monday, May 12, 2014

MAN UNITED YATAFAKARI KUIKOSA ULAYA!

Ryan Giggs anaamini kukosa kucheza Mashindano ya UEFA Msimu ujao ni baraka kwa Manchester United.
Man United walimaliza Msimu huu Nafasi ya 7 na hivyo kukosa kuwemo UEFA CHAMPIONS LIGI na EUROPA LIGI kwa Msimu ujao na hii ni mara ya kwanza tangu Msimu wa 1989/90 kwa Old Trafford kuzikosa Mechi za Ulaya.

Ingawa Giggs, ambae ni Meneja wa Muda wa Man United, amekiri hilo litaathiri sana Wachezaji wasiokuwa na Namba kwenye Timu kwa kukosa Mechi nyingi za kucheza, amebainisha kuwa pengine hiyo ni baraka kwao kwa kucheza Mechi chache Msimu huo mpya na hivyo kujiimarisha na kunufaika kwenye Ligi kama walivyonufaika Liverpool Msimu huu.
Big job: Louis van Gaal has plenty of work to do when he takes over at Manchester United
Giggs amesema: “Unaweza kutazama hilo kwa namna tofauti. Tuna Kikosi kikubwa na baadhi ya Wachezaji wanaweza kukosa nafasi za kucheza kama tupo nje ya Ulaya lakini ikiwa tutafanikiwa kwenda mbali kwenye Vikombe vya England hilo litawasaidia!”
Ryan Giggs kubukia kwenye Klabu yake Old Trafford msimu ujao.

No comments:

Post a Comment