Timu hizo mbili ambazo zimepanda moja kwa moja ni Mabingwa wa Championship, Leicester City, ambao walipanda wakiwa na Mechi 6 mkononi na pia kutwaa Ubingwa mapema Mwezi uliopita, na nyingine ni Burnley ambayo imerejea tena Ligi Kuu England baada ya Miaka mitano walipoifunga Wigan Bao 2-0 hapo Aprili
21.
Katika Mechi hizi za mwisho za Leo, Brighton iliifunga Nottingham Forest Bao 2-1 na kufanikiwa kukukamata Nafasi ya 6 na hivyo kutinga Mechi za Mchujo ikiungana na Derby County, QPR na Wigan ambazo zilishachukua Nafasi za 3, 4 na 5.
Timu hizo 4 ambazo zitatinga Mechi za Mchujo zitafanyiwa Droo maalum kupanga Mechi mbili za Mtoano na Washindi wake kukutana Fainali Wembley na Mshindi kupanda Daraja na kucheza Ligi Kuu England Msimu ujao.
Timu za Kushuka Daraja
Tayari, Timu ya Mkiani, Yeovsil, imeshashuka Daraja tangu mwishoni mwa Mwezi Aprili pamoja na Barsley na Timu moja nyingine ambayo Leo imeungana nazo ni Doncaster ambayo ilifungwa na 1-0 na Mabingwa Leicester City huku Birmingham City wakinusurika baada kusawazisha Bao Dakika za mwisho walipotoka 2-2 na Bolton Wanderers.
No comments:
Post a Comment