BUKOBA SPORTS

Tuesday, May 13, 2014

MCHUJO KUPANDA LIGI KUU ENGLAND: FAINALI QPR v DERBY WEMBLEY!! KATI YAO MMOJA KUUNGANA NA LEICESTER NA BURNLEY!

QPR walitoka nyuma kwa Bao 1 na kuifunga Wigan Bao 2-1 na wao kutinga Fainali ya Mechi za Mchujo za Daraja la Championship za kusaka Timu 1 itakayoungana na Leicester City na Burnley kucheza Ligi Kuu England Msimu ujao.
Kwenye Fainali hiyo, QPR itakutana na Derby County ambayo Juzi iliibwaga Brighton Jumla ya Bao 6-2 katika Mechji mbili baada kuichapa 4-1 kwenye Mechi ya Pili.Party time: QPR fans invade the pitch to celebrate their side reaching Wembley
Mechi hizi za Mchujo za Klabu za Daraja la Championship huko England zinahusisha Klabu zilizomaliza Nafasi za 3 hadi 6 kusaka Timu moja kuungana na Mabingwa wa Daraja hilo, Leicester City, pamoja na Timu ya Pili, Burnley, kucheza Ligi Kuu England Msimu ujao.Joy: QPR fans celebrate Austin scoring against Wigan in Champiuonship play-off semi-final
QPR na Wigan zilitoka Sare ya 0-0 katika Mechi ya Kwanza.
Wigan walitangulia kufunga katika Dakika ya 9 na QPR, chini ya Meneja Mkongwe Harry Redknapp, ilisawazisha Kipindi cha Pili kwa Penati ya Austin ambayo ilitolewa na Refa Mark Clattenburg baada Gary Caldwell kumwangusha Hoilett.Rivals: QPR boss Harry Redknapp chats with Wigan manager Uwe Rosler before the match
Bao la ushindi la QPR lilifungwa tena na Austin katika Kipindi cha Kwanza cha Dakika za Nyongeza 30, kwenye Dakika ya 96.
On the ball: QPR forward Junior Hoilett takes on the Wigan defence at Loftus Road
QPR na Derby County zitacheza Fainali Uwanjani Wembley hapo Mei 24 kupata Timu moja nay a 3 kupanda Daraja kucheza Ligi Kuu England Msimu ujao.
Watching on: Sportsmail's Jamie Redknapp (front row) and QPR owner Tony Fernandes (centre) in the crowd
RATIBA/MATOKEO:
Mechi za Pili

[Kwenye Mabano Jumla ya Mabao kwa Mechi mbili]
Jumapili Mei 11
Derby County 4 Brighton and Hove Albion 1 [6-2]
Jumatatu Mei 12.
Queens Park Rangers 2 Wigan Athletic 1 [2-1]
Jumamosi Mei 24
17:00 Fainali - Wembley Stadium
Derby County vs QPR

No comments:

Post a Comment