BUKOBA SPORTS

Sunday, May 11, 2014

NIGERIA KIBOKO SOKA LA VIJANA, YAINYUKA 2-0 NGORONGORO HEROES TAIFA

Na Baraka Mpenja wa fullshangwe, Dar es salaam

MABAO 2-0 waliyopata Nigeria dhidi ya timu ya taifa ya Tanzania ya vijana chini ya umri wa miaka 20,Ngorongoro Heroes jioni hii uwanja wa taifa katika Mechi ya kwanza ya raundi ya pili ya michuano ya Afrika kwa vijana yamempa kazi ngumu kocha mkuu John Simkoko kusonga mbele.
Ngorongora walipata nafasi kadhaa za kufunga kipindi cha kwanza, lakini bado ugonjwa wa kutotumia nafasi muhimu unazidi kuitafuna timu hii.
Mshambuliaji Saady Kipanga alishindwa kuonesha makeke yake baada ya kupoteza nafasi kadhaa za kufunga.

Mpaka dakika 45 za kipindi cha kwanza zinamalizika milango ya timu zote ilikuwa migumu, huku kipa namba moja wa Heroes, Aishi Manula akiumia.
Kipindi cha pili, Manula alishindwa kurejea uwanjani na kumpisha kipa namba mbili, Peter Manyika.

Katika Kipindi hicho cha pili Ngorongoro waliingia kizembe na kujikuta wakifungwa mabao mawili na kumaliza mechi kwa kipigo cha nyumbani cha mabao mawili kwa sifuri.

No comments:

Post a Comment