
Msiba huo ni mkubwa katika fani ya mpira wa miguu nchini kwani, Balozi Gomile-Chidyaonga ndiye aliyefanikisha ujio wa timu ya Taifa ya Malawi (The Flames) ambayo Mei 4 mwaka huu ilicheza mechi ya kirafiki na Taifa Stars jijini Mbeya.
TFF tunatoa pole kwa familia ya marehemu Balozi Gomile-Chidyaonga, Ubalozi wa Malawi nchini na Chama cha Mpira wa Miguu Malawi (FAM), na kuwataka kuwa na subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha msiba huo mzito.
Bwana alitoa, Bwana ametwaa jina lake lihimidiwe. Amina.
BONIFACE WAMBURA
OFISA HABARI NA MAWASILIANO
SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)
No comments:
Post a Comment