Manchester United wakicheza Ugenini huko Turf Moor na Burnley, Timu iliyopanda Daraja Msimu huu, wametoka Sare ya 0-0 na hii ni Mechi yao ya 3 ya Ligi Kuu England kwa Msimu mpya bila ushindi.
Kipindi cha Kwanza kilikuwa cha mashambulizi ya huku na huku na Burnley wangeweza kupata Bao pale pasi ya nyuma ya Jonny Evans kwa Kipa wake David De Gea kuwa fupi na kunaswa na Jutkiewicz lakini Kipa De Gea akaokoa.
Man United wangeweza kupata Bao kwenye Kipindi hicho cha Kwanza baada ya mchezo safi wa Mchezaji mpya Angel Di Maria, akiichezea Mechi yake ya kwanza kabisa Man United, kumfungulia njia Robin van Persie ambae shuti lake liliokolewa na Kipa Heaton.
Refa Chris Foy aliwanyima Penati ya wazi Man United wakati Beki wa Burnley Trippier alipomsukuma Ashley Young na kumwangusha ndani ya Boksi.
Kipindi cha Pili Man United walitawala na kunyimwa tena Penati wakati Young alipopiga Shuti na Barnes kuunawa lakini kwa mara ya Pili Refa Chris Foy alipeta.
Hadi mwisho, Burnley 0 Man United 0.
No comments:
Post a Comment