BUKOBA SPORTS

Saturday, August 16, 2014

PREMIER LEAGUE: MANCHESTER UNITED 1 vs 2 SWANSEA CITY, UNITED WAANZA MSIMU KWA KIPIGO! GIGURDSSON IAPA USHINDI SWANSEA.

Rooney alipoifungia bao la kusawazisha kufanya 1-1 kipindi cha pili dakika ya 53
Kipindi cha Pili Meneja wa Man United Louis van Gaal alifanya mabadiliko kwa kumtoa Chicharito na kumuingiza Nani na pia kuubadili Mfumo wao kutoka 3-4-1-2 na kuja 4-4-1-1 kwa Difensi kuwa na Phil Jones, Fulbeki wa Kulia na Ashley Young, Fulbeki wa Kushoto, Masentahafu kuwa Smalling na Blackett na hilo lilileta mafanikio kwao.

Dakika ya 53 kipindi cha pili kapteni wayne Rooney anaisawazishia bao na kufanya 1-1baada ya kupigwa kona na mabeki wa Swansea kujichanganya na hatimaye Rooney kutupia bao kwa tiktaka na ikiwa ni baada ya muda mfupi man United kufanya mabadiliko kwa kutoa 'Chicharito' Hernandez na kuingia Nani. Dakika ya 72 kipindi cha pili Gylfi Sigurdsson ndie aliyewafungia bao la kuongoza Swansea na mtanange kumalizika kwa 2-1 dhidi ya Man United.Swansea City's Ki Sung-yueng scores his side's first goalDakika ya 28 kipindi cha kwanza Sung-Yong Ki alipowachoma man United bao.
Dakika ya 28 kipindi cha kwanza Sung-Yong Ki anawapachikia bao na kufanya 1-0 dhidi ya wenyeji Manchester United baada ya kupata pasi safi kutoka kwa Gylfi Sigurdsson. Kipindi cha kwanza kilimalizika Swansea City wakiwa mbele ya bao 1-0 dhidi ya Wenyeji Manchester United.Kocha Van Gaal anaamini kwa Vijana wake na amewapa nafasi kubwa katika Mtanange huu wa Ufunguzi wa Ligi kuu England msimu wa 2014/15 ambao punde wanaanza kucheza kwa kuikaribisha Swansea City Nyumbani Old Trafford. Blackett na  Lingaard wanaanza katika kikosi cha kwanza.
VIKOSI:
Kikosi cha Swansea
Fabiański; Rangel, Williams, Amat, Taylor, Ki, Shelvey, Dyer, Sigurðsson, Routledge, Bony.
Akiba: Tremmel, Bartley, Richards, Tiendalli, Montero, Sheehan, Gomis.
Kikosi cha Man United
De Gea, Jones, Smalling, Blackett, Lingaard, Fletcher, Herrera, Young, Mata, Rooney (c), Hernandez
Akiba: Amos, James, M Keane, Fellaini, Kagawa, Nani, Januzaj

No comments:

Post a Comment