Kipindi cha pili dakika ya 50 Pepe ndie aliyetupia kambani bao la pili na kufanya Real kuongoza 2-1 dhidi ya Barcelona akipewa pasi na Toni Kroos.
Dakika ya 61 Karim Benzema aliifungia bao la tatu Real na kufanya 3-1 dhidi ya Barcelona. Ni baada ya kuwatoka Mabeki wa Barcelona na kutokea chenga safi ya James Rodríguez na kumwachia Karim Benzema aliyemaliza kazi kwa kuziona nyavu na kupata bao la tatu kwenye Uwanja wa Estadio Santiago Bernabéu wakiongozwa na mwamuzi Jesús Gil na mbele ya mashabiki wapatao 85450.
Ushindi huu unawapandisha Real nafasi ya pili wakiwa na pointi 21 nyuma ya pointi moja ya Vinara Barca ambao wana pointi 22 kileleni.
1-1 Cristiano Ronaldo anaswazisha kwa mkwaju wa Penati katika dakika ya 35 kipindi cha kwanza. Ni baada ya Piqué Kuunawa mpira uliopigwa na Marcelo ndani ya kumi na 18 (Box). Hadi Mapumziko Real madrid 1, Barcelona 1.
VIKOSI:
Real Madrid: Casillas, Carvajal, Ramos, Pepe, Marcelo, Kroos, Modric, Isco, James, Ronaldo, Benzema
Akiba: Navas, Varane, Khedira, Hernandez, Arbeloa, Nacho, Illarramendi
Barcelona: Bravo; Alves, Piqué, Mascherano, Mathieu; Xavi, Busquets, Iniesta; Messi, Suarez, Neymar
Akiba: Ter Stegen, Rakitic, Pedro, Bartra, Alba, Roberto, Munir
No comments:
Post a Comment