Samuel Eto'o akishangilia bao lake la dakika za mwisho kwenye dakika ya 82 baada ya kuisawazishia bao Everton kwa kuweka 1-1 dhidi ya Krasnodar na mpira huo kumaliza kwa sare hiyo.
Eto'o aliweka sare hiyo huku kipute hicho kikionekana kuelemea upande mmoja na kuonekana kama mpira huo ungelimalizika kwa 1-0 lakini la!
Patashika kwenye lango Wachezaji wa Everton wakionekana kufanya bidii ya kutafuta bao
Mchezaji wa Krasnodar Ari ndie aliyewafungia bao hilo na kufanya 1-0 kipindi cha kwanza dakika ya 42 kwenye Uwanja wa Kuban.
Ariakishangilia na kupongezwa na kocha Oleg Kononov kwenye Europa ligi Kundi H ambapo wao
Everton walishinda Mechi yao ya kwanza bao 4-1 dhidi ya Klabu ya Germany Wolfsburg, Na leo hii walikuwa Ugenini kucheza na FK Krasnodar ya Urusi ambako wamemaliza mtanange huu kwa sare ya 1-1 na mchezo wa kwanza wa timu hiyo ya Urusi walitoka sare pia ya bao 1-1.
aliyewapa bao Krasnodar Ari akishangilia bo lake la dakika ya 42.
Kipa wa Everton Tim Howard akishangilia bao baada ya kusawazisha timu yao kwa kuweka 1-1
Patashika likiendelea...
Mashabiki wa Urusi wakiipamba FC Krasnodar
Phil Jagielka akichuana na mchezaji wa Krasnodor Ricardo Laborde kipindi cha pili.
No comments:
Post a Comment